URAIA NA MAADILI | MOCK WILAYA YA ROMBO

Bongo Life

 

HALMASHAURI YA WILAYA YA ROMBO

MTIHANI WA MOCK

DARASA LA VII

SOMO: URAIA NA MAADILI

1.     Kama mtoto unayeishi katika nyumba yenye ukandamizaji wa kijinsia je ni hatua gani inaweza kutumika katika kutokomeza ukandamizaji wa kijinsia _____ A)Kutoa elimu kwa wote B) Kutoa elimu kwa wanaume C) Kutoa elimu kwa watu wazima D) Kutoa elimu kwa watoto E) Kutoa elimu kwa vijana

2.     Kitendo cha mtoto wa kike kumsimulia baba yake jinsi anavyoepuka kushawishiwa kufanya ngono na kijana wa kiume kinaitwa_______
A) Kujijali B) Uaminifu C) Uwazi D) Nidhamu Binafsi E) Ustahimilivu

3.     Kama Mwanafunzi mwenye kujitolea katika kufanya kazi mbalimbali za shuleni na jamii utatumia mbinu ipi kuwafanya wanafunzi wenzako wajitolee kama wewe ______ A) Kuwashurutisha B) Kuwatumikisha C) Kuwahamasisha
D) Kuwafuatilia E)Kuwaongoza

4.     Mojawapo ya vitendo si vya kawaida kwa mila na desturi za mtanzania _____ A)Watoto Kuwaheshimu watu wazima B) Watoto kuwakaripia watu wazima
C) Watoto  kuwasaidia wazee kubeba mizigo D) Watoto kuwaslimia watu wazima E) Kuishi vizuri na wanafamilia

5.     Wanawake na wanaume wanawajibu na majukumu tofauti katika jamii. Ni neno gani linafafanua wajibu na majukuu hayo?______
A) Stadi B) Jinsia C) Jinsi D) Morali E) Usawa

6.     Mahusianao mabaya baina ya wanajamii yanaleta matokeo hasi katika jamii zetu.Nini athari ya kunyanyapaa_____ A) Kukosekana kwa amani na usalama
B) Kuimarika kwa upendo na urafiki C) Kuongezeka kwa umaskini na ujinga
 D) Kuongezeka kwa migogoro na mapigano E) Kukuza urafiki na uvumilivu

7.     Mkuu wa Shule ya Msingi Lemosho ameanzisha kitendo cha ushauri nasaha katika shule yake. Nini umuhimu wa kitengo hicho ______A) Kutoa muongozo wa jinsi ya kutatua changamoto B) Kueleza matatizo ya wanafunzi hadharani
 C) Kuwashauri wanafunzi wenye matatizo kujieleza D) Kuwatangaza wanafunzi wenye matatizo E) Kuwatenge wanafunzi wenye matatizo

8.     Bwana mnyonge ni Afisa maendeleo wa kijiji cha Mlima ni ambaye huwaelimisha wanakijiji kuhusu majukumu ya kijamii. Ni jukumu lipi kati ya yafuatayo ni la kijamii:- _______ A) Kumwagilia bustani ya Familia B) Kufagia na kudeki nyumba C) Kusafisha chumba cha Kulala D) Kushiriki katika ujenzi wa Shule E) Kulisha Mifugo ya Nyumbani

9.     Rasilimali za Taifa ni tunu zinazotakiwa kutunzwa na kuhifadhiwa nani ana wajibu wa kutunza na kuhifadhi _______ A) Maafisa wa Polisi B) Maafisa wa jeshi C) Raia wote D) Baba na Mama E) Viongozi wote wa serikali

 

 

 

 

10.   Kukubali kukosolewa ni jambo la hekima sana. Onyesha sentensi sahihi kati ya hizi _______ A) Kukosolewa ni vibaya B) Tukubali kukosolewa tunapofanya makosa
C) Kukosolewa huleta ugomvi D) Anayekosea asikosolewe E) Tusikubali kukosolewa

11.   Kiongozi mmoja alikaa madarakani kwa muda mrefu pasipo kuacha huku akijirimbikizia. Je hali ya kiongozi kujikusanyia madaraka ya kila kitu huitwa?
_____ A) Uwazi B) Ukiritimba C) Umaskini D) Ujinga E) Utandawazi

12.   Chombo chenye mamlamka ya kumwondoa Rais madarakani kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni ______  A) Spika wa Bunge
B) Waziri Mkuu C) Mkuu wa Wilaya D) Mkuu wa Mkoa E) Wabunge

13.   Jumuiya ya Afrika Mashariki awali ilikuwa na nchi au wanachama sita kabla ya jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo kujiunga. Je nchi hii ilijiunga mwaka gani? ________ A) 1977 B) 2000 C) 2022 D) 2020 E)1967

14.   Mwenge wa Uhuru huitambulisha Tanzania kama nchi huru. Ukiwa kama mtanzania unadhani huo mwenge uliwashwa na kupandishwa katika mlima Kilimanjaro tarehe na mwaka gani?____ A) 26 April 1964 B) 9 December 1962
 C) 8 Disemba 1961  D) 26 April 1962 e) 9 Disemba 1961

15.   Rais ndiye anayefanya uteuzi na kutengua viongozi kati ya wafuatao yupi ambaye hateuliwi na Rais ________ A) Mawaziri B) Wakuu wa Mikoa
C) Wakuu wa Wilaya D) Spika wa Bunge E) Mwanasheria Mkuu wa Serikali

16.   Jeshi la Zimamoto lilianzishwa mwaka 2007,ukitaka kupata msaada wa jeshi hilo unapaswa kupiga simu namba ipi?____ A) 113 B) 114 C) 311 D) 511 E) 411

17.   Mama Sophia anapenda mwanae achangamane na wenzake. Unafikiri lipi sio tendo la kumshirikisha mwanae na wenzake?______ A) Kula B) Kucheza
 C) Kusoma D) Kusaidiana E) Kubebwa na mama yake

18.   Kwanini watu wengi hupenda kutupa taka katika jaa_____ A) kuogopa muonekano B)kuogopa kuadhibiwa C) kuondoa uchafu katika  mazingira D)kuogopa kukiuka mila na desturi E) kuogopa uzalendo

19.   Makosa ya Kimtandao yanakithiri siku hadi siku Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilitunga sheria ya makosa ya mtandao mwaka gani?_________
 A) 2019 B)2020 C)2015 D)2010 E)2014

20.   Kila mtu lazima awe mvumilivu ili kukabili changamoto kipi kati ya vifuatavyo siyo kitendo cha uvumulivu katika jamii_____  A) Kuwa na subira B) Kuwa jasiri na kuongea mbele za watu C) Kuomba na kutoa msamaha D) Kufuata sheria za kuwasilisha  malalamiko E) Kutofanya migomo

21.   Ili mipango iwe na ufanisi unapaswa kufuata hatua za utekelezaji mojawapo siyo faida ya kufuata hatua za utekelezaji wa mipango______ A) Kutambua rasilimali B) Kuongeza ufanisi C) Kutoa Rushwa D) Kujiamini E) Matumizi mazuri ya muda

22.   Mwanafunzi hufanya kazi zake kwa nadharia na vitendo ili kuelewa zaidi, Je hutumia milango gani ya fahamu ili kufanikiwa _____ A) Pua na Mdomo
 B) Milango yote ya fahamu C) Macho na Ngozi D) Pua na Ulimi E) Ngozi na Midomo

 

 

 

 

23.   Haki za kibinadamu ni huduma anayopaswa binadamu kupata kipi sio chombo cha utetezi sio chombo utetezi wa haki za binadamu_____ A) Katiba ya Nchi
 B) TAKUKURU C) Vyombo vya habari D) Tume ya haki za Binadamu
E) Bunge la Tanzania

24.   Kukua kwa Utandawazi katika jamii yoyote huwa na manufaa na madhara yake. Nini madhara ya Utandawazi katika jamii______ A) Kuwepo kwa mmomonyoko wa maadili B) Kudumaa kwa teknolojia ya habari C) Kupungua kwa mwingiliano wa watu D) Kupungua kwa fursa za ajira E) Kudumishwa kwa huduma za jamii

25.   Ni kwa namna gani mafundisho ya kijamii husaidia kutawala hisia mbaya na mihemko kwa vijana _______ A) Hisisitiza amani, Upendo na Kusameheana
B) Hujenga, matatizo chanya katika kutatua changamoto C)Husisitiza kufanya mazoezi ya mwili na akili D) Husisitiza kushiriki katika kutatua matatizo ya
wengine E) Husaidia kutafuta taarifa juu ya matatizo ya jamii

26.   Kiongozi Mkuu wa shughuli za serikali Bungeni ni Waziri Mkuu. Ipi kati ya zifuatazo ni sifa ya Waziri Mkuu ______ A) Lazima awe Msomi B) Lazima awe Mwanaume C) Lazima awe Mbunge D) Lazima awe Mwana CCM E) Lazima achaguliwe na Wananchi

27.   Zifuatazo ni vitendo ambavyo vinalenga  kulinda uhuru na umoja wa kitaifa isipokuwa _____ A) kuheshimu sheria za nchi B) kulinda mipaka ya nchi 
C) kuheshimu haki za binadamu D) kuondoa matendo maovu  E)kuheshimu viongozi

28.   Ipi kati ya zifuatazo si faida za kubuni njia mbadala  katika kukabiliana na tatizo:-______A) Husaidia kutatua changamoto iliyoshindikana B) Husaidia kutatua tatizo lililokosa ufumbuzi C) Husaidia kupata utatuzi wa tatizo jipya D)Husaidia kupata muda wa ziada wa kujifurahisha na kujitafakari E) Kuweza kusaidia kufika malengo

29.   Malengo ni dhamira au kusudio la kutelekeza jambo lililopangwa. Je, kuna aina kuu ngapi za malengo_____ A) Tatu B) Mbili C) Nne D) Tano E) Moja

30.   Mambo yote lazima yafanyike kwa utaratibu maalumu. Je, mambo yanayopaswa kukamilika kabla ya mengine hujulikana kama________
 A) Mwanzoni B) Vipanyuma C)Muktadha D) Vipaumbele E) Ving’ang’anishi

31.   Mtu mnafiki lazima asiruhusiwe kuiongoza jamii. Utamtambuaje mnafiki katika jamii ______ A) Huchonganisha watu B) Husema kweli C) Huwa na uhakika na ayasemayo D) Anawachonganisha watu E) Anapenda suluhu

32.   Watu wote wanapaswa kuheshimiana na kusaidiana. Kipi kati ya vifuatavyo ni kitendo cha kuharibu uhusiano baina ya watu______ A) Kutothamini wengine
B) Kuwaonya wengine C) Kufanya kazi kwa bidii D) Kusema Ukweli
E) Kusaidiana

33.   Nchini Tanzania kila baada ya miaka kumi hufanyika zoezi la Sensa la uhesabuji wa watu na makazi. Je mwaka huu sensa hufanyika tarehe ngapi?______
 A) 23 Agosti 2022 B) 27 Agosti 2022 C) 20 Octoba 2020  D) 23 Julai 2021  E) 29 October 2022

 

 

 

 

 

34.  Mihimili ya dola hutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa katiba ya Tanzania. Je, Askari polisi alimpiga Raia na kumuua bila kukusudia shauri lake  litaamuliwa na muhimili upi wa dola ______  A) Baraza la Mawaziri B) Bunge
C) Serikali D) Mahakamani E) Katiba ya Tanzania

35.  Elimu ya afya ya Uzazi ni muhimi kwa manufaa ya watoto wetu. Elimu hiyo inahusisha vitu vifuatavyo isipokuwa______  A) Ujauzito B)Ukuaji  na Kubalehe C) Magonjwa ya Mlipuko D) Masuala ya Hedhi E) Uzazi wa mpango

36.  Mali za umma lazima zitunze kwa manufaa ya watanzania. Kipi kati ya vifuatavyo si kitendo cha matumizi ya mali za umma _____A) Rushwa
 B) Ufisadi C) Mikataba mibovu D) Kutojali mali za umma E) Kuchagua viongozi kwa kupiga kura

37.  Uhusiano mzuri katika jamii huleta amani na utulivu. Ni kipi kati ya vifuatavyo kinadumisha uhusiano mzuri baina ya watu wenye tamaduni tofauti_____
A) Kusalimiana B) Aina ya mavazi C) Aina ya Chakula D) Matumizi ya Lugha E) Shughuli za kiuchumi

38.  Kwa sheria tume ya Uchaguzi Tanzania mgombea kwa nafasi ya uraisi ni lazima awe na umri usiopungua miaka ____A) 21 B) 31 C) 40 D) 41 E) 45

39.  Mikakati gani ifanyike ili kuzuia watu wenye tabia ya kuharibu uhusiano mzuri baina ya watu?____ A) Kuwaelimisha umuhimu wa umbea B) Kuwaelimisha juu ya Uongo na Umbea C) Kujenga uelewa juu ya Kuepuka wivu na kusengenya D) Kujenga uelewa juu ya kutokuwa huru kusema uongo
E) Kujenga uelewa juu ya wajibu wa kuigiza na kusengenya

40.  Meya wa halmashauri huchaguliwa kutoka kwenye kundi fulani la watu. Je kundi hilo ni _______ A) Wabunge B) Madiwani C) Mawaziri D) Wakuu wa Wilaya E) Wananchi

 

SEHEMU: B (ALAMA 10)

Katika swali la 41 – 45 andika majibu sahihi katika nafasi zilizoachwa wazi kwenye fomu ya kujibia uliyopewa (OMR) kwa kutumia kalamu ya wino wa bluu au mweusi

41.  Chombo chenye mamlaka ya kumshauri Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni ________________________

42.  Vitu muhimu na vya thamani vinavyomilikiwa na mtu shirika, au Serikali hujulikana kama ___________________

43.  Katika jamii zetu baadhi ya mila huathiri sana wanawake, mojawapo ya mila hizi ni ukeketaji. Eleza madhara mawili yanayotokana na ukeketaji wa wanawake  __________________

44.  Wahitimu wa darasa la saba walisoma somo la uraia na maadili wanawezaje kuinufaisha jamii zao kwa elimu hiyo waliyoipata_____________________

45.  Eleza faida zozote mbili za serikali ya Kidemodrasia___________________

Post a Comment

0Comments

Post a Comment (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Check Now
Accept !